Tuesday, July 12, 2016
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limemkamata Askofu
wa Kanisa la Ufufuo na Uzima, Josephat Gwajima, Uwanja wa Ndege wa
Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA), baada ya kushuka katika ndege ya
Shirika la Ndege la Kenya (Kenya Airways) akitokea nchini Kenya.
Askofu Gwajima, alikamatwa jana asubuhi na makachero wa Jeshi la
Polisi waliokuwa wamepiga kambi eneo hilo, baada ya kupata taarifa za
kuwasili kwake.
Vyanzo vya habari kutoka kwa watu wa karibu na Askofu Gwajima,
vilisema kuwa baada ya kiongozi huyo wa kiroho kushuka katika ndege,
alitakiwa kupanda helikopta yake ili aelekee Hoteli ya Sea Cliff iliyopo
Masaki, Dar es Salaam kwa ajili ya mapumziko.
Kabla ya kuanza safari ya kuelekea Sea Cliff, Askofu Gwajima,
alijikuta akiishia mikononi mwa polisi na kupelekwa moja kwa moja Kituo
Kikuu cha Polisi, Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kwa ajili ya kuhojiwa
Vyanzo hivyo vilidai kuwa baada ya kufikishwa kituoni, alipelekwa kwa
Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Simon
Sirro na baadaye ofisi ya Mkuu wa Upelelezi wa kanda hiyo, Camillus
Wambura.
“Askofu Gwajima alikamatwa uwanja wa ndege na polisi akitokea nje ya
nchi na kufikishwa Kituo Kikuu cha Polisi cha Kanda Maalumu na kuhojiwa,
lakini ameachiwa kwa dhamana na simu zake za kiganjani zinashikiliwa
kwa ajili ya uchunguzi,” kilisema chanzo hicho.
Msemaji wa kiongozi huyo wa kiroho, Yekonia Behagaze, alikiri kiongozi wao kukamatwa.
“Ni kweli Askofu Gwajima amekamatwa na polisi leo (jana) asubuhi akitokea nje ya nchi, alihojiwa kwa saa nne,” alisema.
Alisema baada ya kumaliza mahojiano hayo, aliachiwa kwa dhamana ili aendelee na majukumu yake.
Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Sirro, alithibitisha kukamatwa kwa Askofu Gwajima.
“Ameletwa, amehojiwa, amepewa dhamana na uchunguzi unaendelea,” alisema.
Chanzo: Mtanzania.
Related Posts
Donny Roberty Mshindi Miss Mwanza 2016 Tazama Picha hapa chini.
Usiku wa jana Ijumaa Agost 19,2016 kuamkia leo Jumamosi Agost 20,20...
MAONESHO YA BIASHARA ROCK CITY MALL MWANZA.
Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda n...
TFF Yatoa Angalizo Kwenye Msimu Mpya Wa VPL 16-17.
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2016/17 inatarajiwa kuan...
Sumatra Imesema hakuna usafiri utakaositishwa.
MAMLAKA ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) imewatoa hofu ...
Hesabu inaendelea Ibra aweka mbili Nyumbani (VIDEO).
Endeleeni kuhesabu, ndiyo lugha rahisi unayoweza kuitumia baada...
Mambo 8 Yatakayokusaidia Kufikia Malengo Yako.
Kila wakati wengi wetu katika maisha, ni watu wa kujiwekea malengo....
Mkurugenzi Atishia Kuitisha Daftari la Mahudhurio saa tisa Usiku sababu Je?
Normal 0 false false false EN-U...
Baada ya Cameroon huyu ndio kuwa Waziri mkuu wa Uingereza.
Katika saa au siku kadhaa zijazo, Waziri wa maswala ya nda...
ULIPITWA; MATOKEO YA ENGLAND VS RUSSIA YAKO HAPA.
June 11 2016 michuano ya Euro 2016 inayofanyika Ufaransa imeen...
- Blogger Comments
- Facebook Comments
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment