Monday, August 8, 2016
Mbio za Mwenge wa Uhuru zimetua
Kanda ya ziwa huku zikizua sintofahamu kwa watumishi wa umma waliotakiwa
kutokukosa mkesha wake ili kukwepa rungu la Mamlaka za kinidhamu dhidi yao.
Taarifa kutoka wilayani Sengerema
zilieleza kuwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya hiyo ameagiza watumishi wote
wa wilaya hiyo kuhakikisha wanahudhuria mkesha huo na kwamba daftari la
mahudhurio litaitishwa majira ya saa 6 usiku, saa 9 usiku na saa 12 usiku.
Hayo yamebainishwa katika Tangazo
rasmi lililosainiwa na Msangi M.A kwa niaba ya Mkurugenzi, Magessa Boniface.
Aidha, katika Wilaya ya Nyamagana
mkoani Mwanza, imeelezwa kuwa walimu wakuu wa shule za msingi na sekondari
waliitwa katika kikao na Mkuu wa Wilaya hiyo, Mary Tesha ambaye aliwaeleza kuwa
ambaye hatahudhuria mkesha huo atakumbwa na adhabu ikiwa ni pamoja na kushushwa
vyeo.
Hata hivyo, Mkuu huyo wa Wilaya
alipotafutwa, alikana kuwaeleza walimu hao kuwa wangeshushwa vyeo kama
wasingehudhuria ingawa alikiri kuwa alikutana nao.
“Sijasema hayo, nilichosema ni kuwa
Mwenge ni jukumu letu watumishi tunapaswa kushiriki. Hao walimu ni wajumbe wa
Kamati za Mbio za Mwenge hivyo wanapaswa kushiriki. Hilo la kufukuza,
kuwawajibisha hapana,” alisema Tesha.
Katibu wa Chama cha Walimu Tanzania
(CWT) wilaya ya Nyamagana, Asha Juma alisema kuwa ingawa amesikia kuwepo kwa
maagizo hayo, hajapata malalamiko kutoka kwa walimu.
“Najuwa wanahamasisha watumishi
waende, lakini nadhani wangetafuta njia nyingine ya kuwahamasisha sio vitisho,”
alisema Katibu huyo wa CWT.
Related Posts
Donny Roberty Mshindi Miss Mwanza 2016 Tazama Picha hapa chini.
Usiku wa jana Ijumaa Agost 19,2016 kuamkia leo Jumamosi Agost 20,20...
MAONESHO YA BIASHARA ROCK CITY MALL MWANZA.
Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda n...
TFF Yatoa Angalizo Kwenye Msimu Mpya Wa VPL 16-17.
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2016/17 inatarajiwa kuan...
Sumatra Imesema hakuna usafiri utakaositishwa.
MAMLAKA ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) imewatoa hofu ...
Hesabu inaendelea Ibra aweka mbili Nyumbani (VIDEO).
Endeleeni kuhesabu, ndiyo lugha rahisi unayoweza kuitumia baada...
Mambo 8 Yatakayokusaidia Kufikia Malengo Yako.
Kila wakati wengi wetu katika maisha, ni watu wa kujiwekea malengo....
Gwajima atiwa Nguvuni na Polisi Dar, Imekuaje?
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limemkamata ...
Baada ya Cameroon huyu ndio kuwa Waziri mkuu wa Uingereza.
Katika saa au siku kadhaa zijazo, Waziri wa maswala ya nda...
ULIPITWA; MATOKEO YA ENGLAND VS RUSSIA YAKO HAPA.
June 11 2016 michuano ya Euro 2016 inayofanyika Ufaransa imeen...
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Duuuuuh. kama ndo hivo shida ndo kitu ambachooo. watu sometime tunaishi kwa nidham ya uwoga sana na tutajikuta tu tunafeli kusonga
ReplyDelete