Msanii
mkongwe wa Bongo Fleva, Dudu baya ametoa maoni yake kuhusiana ongezeko la label
za muziki Bongo, ambapo amesema ni jambo zuri ila tatizo wasanii wanaosimamiwa
na label hizo.
Akiongea
kwenye kipindi cha Planet Bongo cha Ea Radio, Dudubaya amesema wasanii wengi wa
bongo wanaingia mikataba wasiyoridhika nayo ili kupata umaarufu na baadaye
wakishafanikiwa wanaanza kuongea maneno machafu kuhusu menejimenti zilizowatoa.
Ametoa
mifano ya Bongo Records enzi Wateule, Dogo janja alivyoondoka TipTop na
kuanza kusema hakuwahi kulipwa chochote pamoja na mifano mingi ya watu
waliojaribu kuanzisha lebel wakaishia njiani.
Ametolea
mifano lebel kama WCB na nyinginezo ambapo ameisema inafanya vizuri lakini
haamini kabisa wasanii wake endapo watadumu
0 comments:
Post a Comment