728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, June 6, 2016

    Faiza Ally: Sipo tayari kurudiana na ‘Sugu’ ila akihitaji mtoto mwingine nipo tayari.



    Muigizaji na mrembo Bongo, Faiza Ally amesema hayupo tayari kurudiana kimapenzi na baba watoto wake ambaye ni Mbunge wa Mbeya mjini Joseph ‘Sugu’ Mbilinyi, ila yupo tayari kuzaa nae mtoto wa pili.

    Akiongea kupitia kipindi cha Kubamba cha Times Fm Jana, bidada huyo Mama wa mtoto mmoja aitwae Sasha amedai hamkumbuki Sugu kwa kuwa hakuwa ‘Romantic’ na alizo nazo kwake ni hisia tu za kupata mtoto wa pili na yeye.

    “Sitaki kuzaa na kila Mwanaume, nieleweke wazi sitaki kurudiana na Sugu ila akinifata akidai anataka tuzae mtoto wa pili nipo tayari” Alisema.

    Katika ‘line’ nyingine Mama Sasha alisema anajutia kitendo chake cha kutokutumia kinga alipojamiiana na Baba mtoto wake huyo kitendo ambacho kilisababisha kupata Ujauzito.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Faiza Ally: Sipo tayari kurudiana na ‘Sugu’ ila akihitaji mtoto mwingine nipo tayari. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top