Thursday, September 3, 2015
Maandalizi ya mchezo kati ya Tanzania (Taifa Stars) dhidi ya Nigeria
(Super Eagles) yamekamilika, ambapo leo Shirikisho la Mpira wa Miguu
nchini (TFF) limetangaza viingilio vya mchezo huo wa jumamosi kati huku
kiingilio cha chini kabisa kikiwa shilingi elfu saba tu.
Viingilio vya mchezo huo wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa ya
Afrika (AFCON Qaulifier 2017) kundi G itakua ni VIP A Tsh 40,000, VIP B
Tsh 30,000, VIP C Tsh15,000, Rangi ya Machungwa (Orange) Tsh 10,000, na
viti vya rangi ya Bluu na Kijani Tsh 7,000.
Tiketi za mchezo huo zinatarajiwa kuanza kuuzwa kesho siku ya ijumaa saa 4 kamili asubuhi katika vituo kumi vifuatavyo:
(i) Ofisi za TFF – Karume
(ii) Buguruni – Oilcom
(iii) Mbagala – Dar live
(iv) Ubungo – Oilcom
(v) Makumbusho – Stendi
(vi) Uwanja wa Taifa
(vii) Mwenge – Stendi
(viii) Kivukoni- Feri
(ix) Posta – Luther House
(x) Big Bon – Msimbazi Kariakooo
TFF inawaomba watanzania, wapenzi na wadau wa mpira wa miguu kununua
tiketi za mchezo huo katika magari yaliyopo kwenye vituo vilivyotajwa
ili kuondokana na tatizo la kuuziwa tiketi zisizokuwa halali.
Jeshi la Polisi nchini kwa kushirikiana na idara nyingine za
kiusalama wameandaa usalama wa kutosha katika kuelekea kwenye mchezo na
kuhakikisha kila mpenzi wa mpira wa miguu anaingia kushuhudia mchezo huo
salama na kuondoka salama.
Mchezo huo utaanza saa 10:30 jioni kwa saa za Afrika Mashariki
utachezeshwa na waamuzi kutoka nchini Rwanda ambao wanatarajiwa kuwasili
leo jioni pamoja na kamisaa wa mchezo huo.
Waamuzi wa mchezo huo ni Louis Hakizimana (mwamuzi wa kati) Honore
Simba (mwamuzi msaidizi), Jean Bosco Niyitegeka (mwamuzi msaidizi),
Abdoul Karim Twagiramukiza (mwamuzi wa akiba) wote kutoka Rwanda na
kamisaaa ni Charles Kasembe kutoka nchini Uganda.
Related Posts
Donny Roberty Mshindi Miss Mwanza 2016 Tazama Picha hapa chini.
Usiku wa jana Ijumaa Agost 19,2016 kuamkia leo Jumamosi Agost 20,20...
MAONESHO YA BIASHARA ROCK CITY MALL MWANZA.
Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda n...
TFF Yatoa Angalizo Kwenye Msimu Mpya Wa VPL 16-17.
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2016/17 inatarajiwa kuan...
Sumatra Imesema hakuna usafiri utakaositishwa.
MAMLAKA ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) imewatoa hofu ...
Hesabu inaendelea Ibra aweka mbili Nyumbani (VIDEO).
Endeleeni kuhesabu, ndiyo lugha rahisi unayoweza kuitumia baada...
Mambo 8 Yatakayokusaidia Kufikia Malengo Yako.
Kila wakati wengi wetu katika maisha, ni watu wa kujiwekea malengo....
Mkurugenzi Atishia Kuitisha Daftari la Mahudhurio saa tisa Usiku sababu Je?
Normal 0 false false false EN-U...
Gwajima atiwa Nguvuni na Polisi Dar, Imekuaje?
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limemkamata ...
Baada ya Cameroon huyu ndio kuwa Waziri mkuu wa Uingereza.
Katika saa au siku kadhaa zijazo, Waziri wa maswala ya nda...
ULIPITWA; MATOKEO YA ENGLAND VS RUSSIA YAKO HAPA.
June 11 2016 michuano ya Euro 2016 inayofanyika Ufaransa imeen...
- Blogger Comments
- Facebook Comments
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment