728x90 AdSpace

Thursday, September 3, 2015

Wakulima Kuandamana Ufaransa.



TIMES FM.
Leo nchini ufaransa kunafanyika maandamano toka kwa wakulima na wafugaji kuelekea mji mkuu wa nchi hiyo.
Makamu wa rais wa Shirikisho la Wakulima nchini Ufaransa (FNSEA), Luc Smessaert amesema Kunatrekta zaidi ya 1500 yataelekezwa kwenda Paris pamoja na wakulima na wafugaji zaidi ya 4000 kufanya maandamano kushinikiza unyanyasaji wa sekta ya kilimo kwa wakulima wa nchi ya Ufaransa.
“Bei ya Mazao imekuwa ni ya chini, pembejeo hakuna , wakulima hatuthaminiki pengine haya maandamano yataishtua serikali kutusaidia madai yetu haya ambayo ni kipindi kirefu tumekuwa tukiyapigia kelele”, alisema Luc Smessaert.
Wakulima kutoka wilaya 12 watashiriki katika maandamano hayo katika eneo la taifa. Ujumbe wa wakulima hao utapokelewa leo mchana katika mji wa Matignon, na mwingine utakwenda Bungeni ili kufikisha malalamiko yake kwa wabunge. Maandamano haya yenye ushawishi mkubwa yametajwa kuwa ya kihistoria na wafugaji wengi.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: Wakulima Kuandamana Ufaransa. Rating: 5 Reviewed By: Unknown