728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, September 10, 2015

    Makubwa yaliyojili kimataifa leo nimekuwekea hapa habari za kimataifa zikizoletwa kwako na NAJAT OMARY kupitia taarifa ya habari cg fm radio(AUDIO).



    Yaliyojili hii leo kimataifa Ebana best wangu kama ilivyo kawaida leo nimekuwekea hapa habari zote tatu zinasomwa kwenu na najat omary kupitia taarifa ya habari cg fm radio saa kumi jioni.

    ====
    Mahakama ya Juu nchini RWANDA  itasikiliza pingamizi  lililowekwa na  chama  kikuu  cha  upinzani nchini  humo dhidi ya juhudi  za  Rais PAUL KAGAME kutaka kugombea muhula wa tatu.

    Jaji IMMACULEE NYIRINKWAYA amesema  baada  ya uchunguzi  wa  kina, mahakama hiyo ya juu imepata kila sababu ya  kusikiliza  kesi  hiyo na kutupilia  mbali upinzani  kutoka  serikalini na  kesi  hiyo  imepangwa kusikilizwa tarehe 23 mwezi huu.

    Chama  cha  Democratic Green kinapinga mabadiliko  ya aya  ya  101  ya  katiba  ya RWANDA ambayo  inaweka  ukomo  wa vipindi  vya  urais  kuwa  viwili.

    Rais KAGAME alichaguliwa kwa mara ya kwanza  mwaka  2003  na akachaguliwa  tena  mwaka  2010  na  kwa hiyo  hawezi  kugombea  tena kipindi  cha  tatu.

    Rais  wa  chama  hicho, Bwana FRANK HABINEZA  amesema  wamefurahishwa  na  uamuzi  wa  mahakama  ya juu wa kusikiliza  kesi  hiyo.

    ====

    Kikosi kimoja maalum cha serikali nchini SUDAN kimeshutumiwa kwa kutekeleza mauaji ya halaiki na ubakaji wa raia katika eneo la DARFUR MAGHARIBI tangu mwezi Februari mwaka uliopita.

    Ripoti mpya ya Shirika la kutetea haki za Binadamu inasema kikosi hicho kijulikanacho kama Rapid Support Forces kilitekeleza kile inachosema ni unyama na ukatili katika vijiji tofauti kwenye eneo hilo.

    Walioshuhudia mashambulio hayo wameeleza jinsi vikosi hivyo maalum vya serikali vilivyowakusanya wanavijiji, vikawapiga na kuwabaka wanawake wengi.

    Mmoja wa waathirika alisema alishuhudia wanawake kumi na saba wakibakwa katika hospitali moja.

    Mwingine alisema aliwaona wanawake na wasichana wakibakwa na kisha kuingizwa katika nyumba moja iliyochomwa moto bado wakiwa ndani.

    ====
    NA

    Usafiri wa treni nchini DENMARK umejea tena baada ya  kusitishwa kwenda na kutoka UJERUMANI baada ya kutokuelewana kati ya polisi na mamia ya wahamiaji.

    Kundi moja la wahamiaji lilikataa kushuka katika treni waliyokuwemo kwa madai ya kutaka kusafiri kwenda SWEDEN ambayo ina sheria nzuri ya uhamiaji kushinda DENMARK.

    Polisi wamekuwa wakiwazuia mamia yawahamiaji waliokuwa wakitembea kwa miguu nchini DENMARK kwa lengo la kwenda SWEDEN.

    Habari zinasema baadhi ya wahamiaji wamekuwa wakiwahadaa polisi kwa kujificha katika magari ama katika matrekta yanayokokotwa na farasi.

    NAJJAT OMAR,CGFM

    Bofya play kusikiliza hapa chini best.... 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Makubwa yaliyojili kimataifa leo nimekuwekea hapa habari za kimataifa zikizoletwa kwako na NAJAT OMARY kupitia taarifa ya habari cg fm radio(AUDIO). Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top