728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, September 10, 2015

    UMESIKIA HII KAULI YA MREMA BAADA YA KUKOSA WATU KWENYE KAMPENI ZAKE? NIMEKUWEKEA SOMA HAPA.



    Mwenyekiti Taifa wa chama cha Tanzania Labour Party TLP, na mgombea Ubunge jimbo la Vunjo Augustino Mrema, amelalamikia kuwa anafanyiwa siasa chafu na wapinzani wake.
    Akizungumza na waandishi wa habari jimboni Vunjo, Mrema amepeleka lawama moja kwa moja kwa viongozi wa chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA, kwa kumchafua kwa matusi kwenye kampeni pamoja na kufanyiwa ubaguzi.
    “Siwalaumu wanachama wa CHADEMA, viongozi wao ndio wenye fujo na mimi, sasa najiuliza tatizo ni nini uzee wangu? kama ndio hivyo wawaachie wananchi, kama kuumwa mbona tangu 1984 naugua kisukari, kwa nini wananitendea haya?”
    Katika ‘line’ nyingine, Mzee Mrema amedai bado ana imani na wananchi wa vunjo watampigia kura ili awaongoze kwa mika mingine 5.

    Saa chache baada ya wimbo mpya wa Roma ‘Viva Roma viva’ kutoka September 9, rapper huyo amedai kuwa ametishiwa wimbo huo kufungiwa.

    Kupitia Instagram, majira ya saa mbili usiku Roma aliandika; “WANATAKA KUIFUNGIA NYIMBO YANGU!! KISA TU NIMEONGEA UKWELI!! INANIUMA SANA NATAMANI HATA KULIA NIKIONA UKWELI HAUPEWI NAFASI!! NIOMBEENI NA MNIKUMBUKE KWENYE SALA ZENU NDUGU ZANGU!! Viva Roma viva”

    Bado haijafahamika sababu ya wimbo huo kutaka kufungiwa, na Roma hakupatikana kwenye simu yake nilipomtafuta kwaajili ya kuzungumza nae kuhusu swala hilo. 
    - See more at: http://edwinmoshi.blogspot.com/2015/09/roma-asema-wanataka-kuufungia-wimbo.html#sthash.fq2ksLG0.lCyZ9Ffi.dpuf
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: UMESIKIA HII KAULI YA MREMA BAADA YA KUKOSA WATU KWENYE KAMPENI ZAKE? NIMEKUWEKEA SOMA HAPA. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top