728x90 AdSpace

  • Latest News

    Thursday, September 10, 2015

    WAZAZI AU WALEZI WATAKIWA KUWAPELEKA WATOTO WAO KUJIUNGA NA MAFUNZO YA KUJIANDAA NA KIDATO CHA KWANZA(Audio).



    wazazi na walezi katika manispaa ya TABORA wametakiwa kuwapeleka watoto wao waliomaliza mitihani ya darasa la saba leo kujiunga na mafunzo ya maandalizi  kabla ya kujiunga na elimu ya sekondari mwakani.
    Akizungumza na mussankoningo.blogspot.com mara baada ya kumalizika kwa mtihani wa darasa la saba, Mwalimu Mkuu wa shule ya msingi ISIKE,Bwana CHARLES KALELANDA amesema wazazi kwa sasa wanatakiwa kuwapeleka watoto wao kwenye mafunzo ya maandalizi ya kujiunga na elimu ya sekondari  kwa sababu mtoto akikaa muda  mrefu bila kujifunza akili yake hudumaa.
    Kwa upande wao wanafunzi waliomaliza mitihani yao katika shule za msingi KITETE na ISIKE zilizopo manispaa ya TABORA wamesema matarajio yao ni kufaulu kutokana  na maandalizi mazuri waliyokuwa nayo kabla ya kuingia katika vyumba vya mitihani yao ya mwisho.

    Hata hivyo wanafunzi hao wamewaomba wadogo zao wote wanaobaki shuleni kusoma kwa bidii ili waweze kufaulu katika mtihani wa mwisho na pia kuwaomba  wazazi au walezi wajitahidi  kuwapeleka katika mafunzo ya awali ya elimu ya sekondari.

    Mitihani ya kuhitimu elimu ya msingi ilianza jana na kumalizika leo kote nchinI

    BOFYA PLAY KUSIKILIZA  HAPA CHINI....
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: WAZAZI AU WALEZI WATAKIWA KUWAPELEKA WATOTO WAO KUJIUNGA NA MAFUNZO YA KUJIANDAA NA KIDATO CHA KWANZA(Audio). Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top