728x90 AdSpace

  • Latest News

    Friday, May 20, 2016

    Rais Magufuli Atoa machozi Kufuatia Mauaji ya Watu Watatu Msikitini.


    Rais John Magufuli ametoa salamu za pole kwa wakazi wa mkoa wa Mwanza, kutokana na mauaji ya watu watatu, waliouawa kwa kukatwa mapanga wakiwa msikitini

    Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, jijini Dar es Salaam jana, ilisema Rais Magufuli amesema yupo pamoja na wakazi wa mkoa huo wa Mwanza katika kipindi hiki cha majonzi, kuomboleza watu hao na pia alisema anawaombea wale waliojeruhiwa wapone.

    Wakati huo huo, Wizara ya Mambo ya Ndani imesema imesikitishwa na mauaji ya watu hao watatu, waliouawa msikitini katika wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.

    Kauli hiyo ya Serikali, ilitolewa bungeni mjini Dodoma jana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Masauni Yussuf Masauni.

    Masauni alisema kuwa Serikali inawapa pole wakazi wa Mwanza, viongozi wa mkoa na wilaya ya Nyamagana na mbunge wa jimbo hilo, Stanslaus Mabula.

    Taarifa iliyotolewa na Kurugenzi ya Mawasiliano Ikulu, jijini Dar es Salaam jana, ilisema Rais Magufuli amesema yupo pamoja na wakazi wa mkoa huo wa Mwanza katika kipindi hiki cha majonzi, kuomboleza watu hao na pia alisema anawaombea wale waliojeruhiwa wapone.

    Wakati huo huo, Wizara ya Mambo ya Ndani imesema imesikitishwa na mauaji ya watu hao watatu, waliouawa msikitini katika wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza.

    Kauli hiyo ya Serikali, ilitolewa bungeni mjini Dodoma jana na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Masauni Yussuf Masauni.

    Masauni alisema kuwa Serikali inawapa pole wakazi wa Mwanza, viongozi wa mkoa na wilaya ya Nyamagana na mbunge wa jimbo hilo, Stanslaus Mabula.
    - See more at: http://edwinmoshi.blogspot.com/2016/05/rais-magufuli-atoa-machozi-kufuatia.html#sthash.9sYQEgt6.dpuf
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Rais Magufuli Atoa machozi Kufuatia Mauaji ya Watu Watatu Msikitini. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top