728x90 AdSpace

  • Latest News

    Monday, May 30, 2016

    Wabunge wa Upinzani Wamemgomea Naibu Spika Kwa Kukataa Hoja ya Wanafunzi 7000 Waliofukuzwa UDOM.




    Naibu Spika wa Bunge ameahirisha Bunge kabla ya muda wake baada ya wabunge kutaka kujadiliwa suala la wanafunzi wa Udom kufukuzwa chuoni wakati hawana kosa.

    Mbunge wa Arumeru Mashariki, Joshua Nassari aliomba mwongozo na kutaka sakata la wanafunzi hao lijadiliwe lakini Naibu Spika, Tulia Ackson alisema jambo hilo haliwezi kusitisha shughuli za Bunge hivyo haliwezi kujadiliwa kwa wakati huo.

    Kauli hiyo iliwanyanyua wabunge wa upinzani na baadhi ya wa CCM wakipinga kauli hiyo huku wakiwa wamesimama jambo ambalo lilisababisha kuaihirishwa kwa Bunge hadi saa 10:00 jioni huku akiagiza kukutana kwa kamati ya uongozi ya Bunge
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Post a Comment

    Item Reviewed: Wabunge wa Upinzani Wamemgomea Naibu Spika Kwa Kukataa Hoja ya Wanafunzi 7000 Waliofukuzwa UDOM. Rating: 5 Reviewed By: Unknown
    Scroll to Top