Friday, May 13, 2016
Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Ufaransa, Didier Deschamps ametaja
kikosi cha wachezaji 23, ambacho kitashiriki fainali za mataifa ya
barani Ulaya (Euro 2016) zitakazofanyika kuanzia mwezi ujao.
Deschamps amemuita mshambuliaji wa Arsenal, Olivier Giroud, huku
akimuweka katika kikosi cha kusubiri mshambuliaji Hatem Ben Arfa ambaye
ameonekana kuwa na msimu mzuri akiwa na klabu ya Nice inayoshiriki ligi
ya nchini Ufaransa.
Wengine waliotajwa kwenye kikosi hicho ambacho kitakuwa na jukumu la
kuwa mwenyeji wa fainali za Euro 2016, ni kiungo wa klabu bingwa nchini
England, Leicester City, N’Golo Kante pamoja na kiungo mshambuliaji wa
West Ham Dimitri Payet.
Hata hivyo kocha Deschamps, anatarajiwa kutaja kikosi cha mwisho
atakachoingia nacho mashindanoni Mei 31, ambapo itakua tarehe ya mwisho
ya kuwasilisha majina ya wachezaji wa timu shiriki mbele ya shirikisho
la soka barani Ulaya UEFA.
Kikosi kamili kilichotajwa na kocha Deschamps upande wa makipa
yupo Hugo Lloris (Tottenham Hotspur), Steve Mandanda (Olympique
Marseille) na Benoit Costil (Stade Rennes).
Mabeki: Raphael Varane (Real Madrid), Laurent
Koscielny (Arsenal), Eliaquim Mangala (Manchester City),
Jeremy Mathieu (Barcelona), Patrice Evra (Juventus), Bacary
Sagna (Manchester City), Lucas Digne(AS Roma) na Christophe
Jallet (Olympique Lyon)
Viungo: Paul Pogba (Juventus), Blaise
Matuidi (Paris St Germain), Lassana Diarra (Olympique Marseille), N’Golo
Kante (Leicester City), Yohan Cabaye (Crystal Palace) na Moussa
Sissoko (Newcastle United)
Washambuliaji: Antoine Griezmann (Atletico Madrid),
Dimitri Payet (West Ham United), Anthony Martial(Manchester
United), Kingsley Coman (Bayern Munich), Olivier Giroud (Arsenal) na
Andre-Pierre Gignac(UANL Tigres)
Kikosi cha akiba: Alphonse Areola (Villarreal),
Hatem Ben Arfa (Nice), Kevin Gameiro (Sevilla), Alexandre
Lacazette (Olympique Lyon), Adrien Rabiot (Paris St Germain, Morgan
Schneiderlin (Manchester United), Djibril Sidibe (Lille) na Samuel
Umtiti (Olympique Lyon).
Related Posts
Donny Roberty Mshindi Miss Mwanza 2016 Tazama Picha hapa chini.
Usiku wa jana Ijumaa Agost 19,2016 kuamkia leo Jumamosi Agost 20,20...
MAONESHO YA BIASHARA ROCK CITY MALL MWANZA.
Makamu Mwenyekiti wa Chemba ya Wafanyabiashara wenye Viwanda n...
TFF Yatoa Angalizo Kwenye Msimu Mpya Wa VPL 16-17.
Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara msimu wa 2016/17 inatarajiwa kuan...
Sumatra Imesema hakuna usafiri utakaositishwa.
MAMLAKA ya Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (Sumatra) imewatoa hofu ...
Hesabu inaendelea Ibra aweka mbili Nyumbani (VIDEO).
Endeleeni kuhesabu, ndiyo lugha rahisi unayoweza kuitumia baada...
Mambo 8 Yatakayokusaidia Kufikia Malengo Yako.
Kila wakati wengi wetu katika maisha, ni watu wa kujiwekea malengo....
Mkurugenzi Atishia Kuitisha Daftari la Mahudhurio saa tisa Usiku sababu Je?
Normal 0 false false false EN-U...
Gwajima atiwa Nguvuni na Polisi Dar, Imekuaje?
Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limemkamata ...
Baada ya Cameroon huyu ndio kuwa Waziri mkuu wa Uingereza.
Katika saa au siku kadhaa zijazo, Waziri wa maswala ya nda...
ULIPITWA; MATOKEO YA ENGLAND VS RUSSIA YAKO HAPA.
June 11 2016 michuano ya Euro 2016 inayofanyika Ufaransa imeen...
- Blogger Comments
- Facebook Comments
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 comments:
Post a Comment